Juni 10, 2026 12:28
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

SILINDE ASHIRIKI COP29 NCHINI AZERBAIJAN.

Mhe.David Silinde (Mb), Naibu Waziri wa Kilimo akiambatana na Dkt. Hussein Omary, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula) pamoja na wataalam wengine wa Wizara ya Kilimo wameshiriki katika Mkutano wa 29 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP29) unaofanyika katika mji wa Baku, nchini Azerbaijan.

Katika Mkutano huo, Wizara imeshiriki katika majadiliano na Mwakilishi wa Mfuko wa Ufadhili wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) na kujadili masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na namna ya kuwasilisha miradi ya vipaumbele ya pamoja kwa mfuko huo kwa mwaka 2025.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

MKUU WA MKOA WA MTWARA AZINDUA MINADA YA KOROSHO KWA MSIMU WA 2022/2023 LEO TAREHE 21 OKTOBA KWA VYAMA VIKUU VIWILI TANECU NA MAMCU MKOANI MTWARA.

Peter Luambano

Wajumbe wakiwa kwenye Mkutano wa kimataifa wa korosho uliofanyika Tanzania katika ukumbi wa Mikutano ya kimataifa wa Julius Nyerere

Peter Luambano

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MIKUTANO MUHIMU KUHUSU KILIMO-MAREKANI

Amani Ngoleligwe