Juni 21, 2026 02:49
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

WAKULIMA TANECU WAUZA KOROSHO ZAO KATIKA MNADA WA SITA

Wakulima wa zao la korosho kutoka Chama Kikuu Cha Ushirika TANECU katika mnada wake wa sita uliofanyika Nov 15 2024, wilayani Tandahimba mkoani Mtwara wameuza korosho zao kwa Bei ya juu ya Tsh.3240/= na ya chini ikiwa Tsh.3010=

Jumla ya Tani 17233,875 za korosho ghafi kati 18966,934 zimeuzwa, na zilizobaki ni Tani 1733 ambazo zitauzwa katika mnada wa sita wa Chama Kikuu Cha Ushirika Lindi Mwambao hapo Nov 16-2024.

Mnada huo umefanyika kupitia mfumo wa soko la bidhaa Tanzania (TMX) ukihudhuriwa na maafisa kutoka Bodi ya Korosho Tanzania, viongozi wa TANECU, na wakulima wa korosho kutoka wilaya za Newala na Tandahimba.

Related posts

MAMCU WAUZA KILO 35,445,155 KWA BEI YA JUU SH. 2,510

Amani Ngoleligwe

KOROSHO QUEENS YAPATA UFADHILI WA VIFAA VYA MICHEZO

Peter Luambano

MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA UGAWAJI WA PEMBEJEO KWA MSIMU WA 2023/2024

Peter Luambano