Juni 10, 2026 05:48
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KOROSHO QUEENS YAPATA UFADHILI WA VIFAA VYA MICHEZO

Bodi ya korosho imekabidhi vifaa vya michezo ikiwemo Mipira,Viatu na Sare kwa timu ya mpira ya KOROSHO QUEENS siku ya tarehe 11/05/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Korosho Mtwara,makabidhiano hayo yamefanywa kati ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi Ndug. Gerald Rogathe na uongozi wa KOROSHO QUEENS wakiongozwa na Meneja wa Timu hiyo Ndug. Hussein Omary Kibombwe.

Vifaa hivyo vimetolewa na Bodi ya korosho kwa kuzingatia ombi la ufadhili lililoletwa na KOROSHO QUEENS,aidha kwa kuzingatia umuhimu wa michezo,Bodi imetekeleza ombi hilo kama walivyoleta na pia imewaomba wadau wengine wa michezo kuchangia na kutoa chochote ili kuendeleza ndoto ya timu hii iliyopo mjini Mtwara.

Related posts

HALI YA SOKO LA KOROSHO GHAFI KWA MWAKA 2022/2023

Peter Luambano

BODI YA KOROSHO YAPOKEA TANI 3,680 YA SULPHUR KUPITIA BANDARI YA MTWARA

Peter Luambano

MWONGOZO NA.3 WA UNUNUZI WA KOROSHO KWENYE SOKO LA AWALI KWA AJILI YA WABANGUAJI WA NDANI MSIMU WA 2025/2026

Amani Ngoleligwe