May 28, 2023 04:33
Bodi Ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriMatukioSlider

TANZANIA YAPATA SOKO JIPYA LA KOROSHO BARANI ULAYA

Bodi ya korosho Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imeendelea na juhudi za kuhakikisha wakulima wanafaidika na za zao hili katika maeneo yao hususani kwa kuongeza ajira na kipato kwa kila mkulima wa korosho  Nchini.

Akizungumza katika uzinduzi huo,Kaimu Mkurugenzi Mkuu Ndg.Francis Alfred amesema, juhudi hizi zinatokana na mpango thabiti wa kuongeza kiwango cha korosho inayobanguliwa hapa Nchini hivyo kupelekea ongezeko la thamani ya korosho tofauti na usafirishaji wa korosho ghafi,matokea ya mpango huu ni pamoja na uzinduzi wa usafirishaji wa Korosho zilizobanguliwa kupitia Viwanda vidogovidogo na Vikundi vya wajasiliamali wilayani Tandahimba waastani wa Tani 26 za korosho na Tani Moja ya Nyama ya korosho ambazo zimetafutiwa soko jipya barani Ulaya katika Nchi za Uholanzi na Ujerumani.

Kati ya Tani 26 za korosho hizi,tani 12 na tani moja ya nyama ya mabibo zinasafirishwa kwenda Ujerumani kutoka kikundi cha kina Mama cha TANZANIA DELICIOUS CASHEWS LTD na Tani 14 zinasafirishwa kwenda Nchini Uholanzi kutoka kiwanda cha AMAMA FARMS COMPANY LIMITED,vyote hivi viko wilaya ya Tandahimba-Mtwara.

Akizindua usafirishaji huo,Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba  Mheshimiwa Kanali Patric Swala amesema, nifaraja kubwa kuona mambo kama haya yameanza kujitokeza kwa Nchi yetu na yote hii inatokana na juhudi za serikali yetu pendwa chini ya Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassani,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Related posts

KIKAO CHA SABA CHA BODI YA WAKURUGENZI ROBO YA TATU YA MWAKA

Peter Luambano

MAFUNZO YA UHUISHAJI NA USAJILI WA WAKULIMA WA KOROSHO

Peter Luambano

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred Pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI)-Naliendele Dkt Fortunus Kapinga wamepokea ujumbe wa wageni kutoka Nchini Benin leo tarehe 3 Octoba 2022.

Peter Luambano