Julai 27, 2024 01:13
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KOROSHO QUEENS YAPATA UFADHILI WA VIFAA VYA MICHEZO

Bodi ya korosho imekabidhi vifaa vya michezo ikiwemo Mipira,Viatu na Sare kwa timu ya mpira ya KOROSHO QUEENS siku ya tarehe 11/05/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Korosho Mtwara,makabidhiano hayo yamefanywa kati ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi Ndug. Gerald Rogathe na uongozi wa KOROSHO QUEENS wakiongozwa na Meneja wa Timu hiyo Ndug. Hussein Omary Kibombwe.

Vifaa hivyo vimetolewa na Bodi ya korosho kwa kuzingatia ombi la ufadhili lililoletwa na KOROSHO QUEENS,aidha kwa kuzingatia umuhimu wa michezo,Bodi imetekeleza ombi hilo kama walivyoleta na pia imewaomba wadau wengine wa michezo kuchangia na kutoa chochote ili kuendeleza ndoto ya timu hii iliyopo mjini Mtwara.

Related posts

Wajumbe wakiwa kwenye Mkutano wa kimataifa wa korosho uliofanyika Tanzania katika ukumbi wa Mikutano ya kimataifa wa Julius Nyerere

Peter Luambano

ZIARA YA MASOMO YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAFUNZO YA KILIMO MTWARA-MATI

Peter Luambano

KIKAO CHA KAMATI YA UENDELEZAJI ZAO YA BODI YA KOROSHO TANZANIA

Peter Luambano