Januari 13, 2025 11:56
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KOROSHO QUEENS YAPATA UFADHILI WA VIFAA VYA MICHEZO

Bodi ya korosho imekabidhi vifaa vya michezo ikiwemo Mipira,Viatu na Sare kwa timu ya mpira ya KOROSHO QUEENS siku ya tarehe 11/05/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Korosho Mtwara,makabidhiano hayo yamefanywa kati ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi Ndug. Gerald Rogathe na uongozi wa KOROSHO QUEENS wakiongozwa na Meneja wa Timu hiyo Ndug. Hussein Omary Kibombwe.

Vifaa hivyo vimetolewa na Bodi ya korosho kwa kuzingatia ombi la ufadhili lililoletwa na KOROSHO QUEENS,aidha kwa kuzingatia umuhimu wa michezo,Bodi imetekeleza ombi hilo kama walivyoleta na pia imewaomba wadau wengine wa michezo kuchangia na kutoa chochote ili kuendeleza ndoto ya timu hii iliyopo mjini Mtwara.

Related posts

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Francis Alfred, akizungumza na Wakulima wakati wa ufunguzi wa mnada wa kwanza wa ununuzi wa Korosho Msimu 2023/2024 katika Kijiji cha Mburusa Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Octoba 20,2023

Peter Luambano

MKUTANO MKUU WA WADAU WA TASNIA YA KOROSHO 2024

Peter Luambano

Kikao cha 12 cha Bodi ya Wakurugenzi

Peter Luambano