Aprili 18, 2026 04:30
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MIKUTANO MUHIMU KUHUSU KILIMO-MAREKANI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki katika mijadala muhimu ya kimataifa kuhusu kilimo barani Afrika ambayo ni Africa Agriculture Dialogue (AAD) ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB); na mjadala wa Kimataifa wa Norman E. Borlaug, ulioandaliwa na Taasisi ya World Food Foundation katika mji wa Des Moines, jimbo la Iowa, Marekani, mnamo Oktoba 30, 2024.

Katika hotuba zake, Mhe. Rais Dkt. Samia ameeleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Tanzania ili kuwa mzalishaji mkubwa wa chakula kwa ajili ya kujitosheleza kama Taifa na kuuza Chakula cha ziada kibiashara (feed ourselves, feed others commercially). Aidha, Mhe. Rais Dkt. Samia alibainisha jinsi nchi inavyoimarisha mifumo ya uzalishaji wa chakula kwa kutumia teknolojia za kisasa ili kufikia malengo hayo kama Taifa.


Mikutano hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb); Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo wa Zanzibar, Mhe. Shamata Shaame Khamis (Mb); na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli.

Related posts

TAARIFA FUPI YA MINADA YA KOROSHO ILIYOFANYIKA TAREHE 20 OKTOBA. 2023 A.TANECU LTD KATIKA UKUMBI WA TANDAHIMBA DC

Peter Luambano

BODI YA KOROSHO YAPOKEA TANI 3,680 YA SULPHUR KUPITIA BANDARI YA MTWARA

Peter Luambano

ELIMU YA MAZINGIRA NA HEWA YA UKAA KWA BODI YA WAKURUGENZI

Peter Luambano