Julai 14, 2025 06:02
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

MKULIMA WA KOROSHO KULIPWA SIKU 7 BAADA YA MNADA

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred ametoa ufafanuzi juu ya malipo ya wakulima wa Korosho nchini katika kuelekea msimu huu wa mwaka 2024/2025.

Ndg. Alfred amesema Wanunuzi wa Korosho watalipa fedha kwa vyama vikuu vya ushirika ndani ya siku 5 baada ya mnada kufanyika na Vyama vikuu vinatakiwa kukamilisha malipo hayo kwa wakulima ndani ya saa 48 ambayo ni sawa na siku 2 ili wakulima wapate fedha zao za mauzo, hivyo mkulima atapata malipo yake siku 7 baada ya mnada kufanyika.

Mnada wa kwanza wa Korosho nchini kwa msimu wa mwaka 2024-2025 unatarajiwa kufanyika Oktoba 11,2024 kwa kuanzia na chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU.

Related posts

MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA UGAWAJI WA PEMBEJEO KWA MSIMU WA 2023/2024

Peter Luambano

KIKAO CHA TATHMINI YA UZALISHAJI, MASOKO NA UBANGUAJI WA KOROSHO MSIMU WA 2023/2024

Peter Luambano

TANGAZO KWA WADAU WOTE WA TASNIA YA KOROSHO NCHINI

Amani Ngoleligwe