Wakati minada ya korosho ikiwa inaendelea mkurugenzi wa bodi ya korosho Tanzania ndg Francis Alfred Alfred amewataka wakulima wa korosho nchini kuendelea kudumisha ubora wa korosho ili kuhakikisha kuwa bei ya korosho ghafi inaendelea kuwa nzuri.
Ndg. Alfred ameyasema hayo wakati wa mnada wa kwanza wachama kikuu cha ushirika cha Mtwara, Masasi na Nanyumbu (MAMCU) uliofanyika katika Kijiji cha Nakachindu wilayani Masasi mkoani Mtwara ocktoba 14-2024.
Katika mnada huo wakulima waliuza korosho zao kwa bei ya juu ya Tsh 4195 na bei ya chini ikiwa Tsh 3440, jumla ya tani 18,000 ziliuzwa kupitia mfumo wa soko la bidhaa Tanzania (TMX)
Wakieleza furaha yao ya kuuza korosho zao kwa bei ya juu baada ya miaka kadhaa, wamemshukuru Rasi Dkt Samia Suluhu Hassan kwa utoaji wa pembejeo buree, ambao umewawezesha kupata uzalishaji mzuri wa korosho katika msimu huu wa 2024/2025.
Pia wamemshukuru waziri wa kilimo Hussein Bashe kwa kusimamia na kuhakikisha maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwainua wakulima wa korosho yanatekelezwa ipasavyo.