Machi 17, 2026 07:47
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BODI YA KOROSHO TANZANIA (CBT) YAWATAKA WAKULIMA KUENDELEA KUDUMISHA UBORA WA KOROSHO.

Wakati minada ya korosho ikiwa inaendelea mkurugenzi wa bodi ya korosho Tanzania ndg Francis Alfred Alfred amewataka wakulima wa korosho nchini kuendelea kudumisha ubora wa korosho ili kuhakikisha kuwa bei ya korosho ghafi inaendelea kuwa nzuri.

Ndg. Alfred ameyasema hayo wakati wa mnada wa kwanza wachama kikuu cha ushirika cha Mtwara, Masasi na Nanyumbu (MAMCU) uliofanyika katika Kijiji cha Nakachindu wilayani Masasi mkoani Mtwara ocktoba 14-2024.

Katika mnada huo wakulima waliuza korosho zao kwa bei ya juu ya Tsh 4195 na bei ya chini ikiwa Tsh 3440, jumla ya tani 18,000 ziliuzwa kupitia mfumo wa soko la bidhaa Tanzania (TMX)

Wakieleza furaha yao ya kuuza korosho zao kwa bei ya juu baada ya miaka kadhaa, wamemshukuru Rasi Dkt Samia Suluhu Hassan kwa utoaji wa pembejeo buree, ambao umewawezesha kupata uzalishaji mzuri wa korosho katika msimu huu wa 2024/2025.

Pia wamemshukuru waziri wa kilimo Hussein Bashe kwa kusimamia na kuhakikisha maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwainua wakulima wa korosho yanatekelezwa ipasavyo.

Related posts

MKUU WA MKOA WA MTWARA KANALI AHMED ABBAS AHMED AZINDUA RASMI KOROSHO MARATHON MSIMU WA PILI 2023

Peter Luambano

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred Pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI)-Naliendele Dkt Fortunus Kapinga wamepokea ujumbe wa wageni kutoka Nchini Benin leo tarehe 3 Octoba 2022.

Peter Luambano

MAAFISA KILIMO WA BBT KOROSHO WAENDELEA NA MAFUNZO YA VITENDO

Amani Ngoleligwe