Novemba 3, 2025 03:47
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

SILINDE ASHIRIKI COP29 NCHINI AZERBAIJAN.

Mhe.David Silinde (Mb), Naibu Waziri wa Kilimo akiambatana na Dkt. Hussein Omary, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula) pamoja na wataalam wengine wa Wizara ya Kilimo wameshiriki katika Mkutano wa 29 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP29) unaofanyika katika mji wa Baku, nchini Azerbaijan.

Katika Mkutano huo, Wizara imeshiriki katika majadiliano na Mwakilishi wa Mfuko wa Ufadhili wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) na kujadili masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na namna ya kuwasilisha miradi ya vipaumbele ya pamoja kwa mfuko huo kwa mwaka 2025.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

RULES AND SALES CONDITIONS FOR THE 2023/2024 CROP SEASON

Peter Luambano

Kikao cha ufunguzi wa zoezi la ukaguzi wa hesabu za taasisi Kwa mwaka 2021/2022

Peter Luambano

BODI YA KOROSHO YAZINDUA RASMI MKUTANO WA KIMATAIFA WA KOROSHO 11-13 OCTOBA 2023 JNICC-DAR ES SALAAM

Peter Luambano