Juni 23, 2026 08:26
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KATIBU MKUU MWELI AKUTANA NA IFAD, AFDP

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) na wataalamu kutoka Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) wakiongozwa Mkurugenzi Mkazi, Bw. Mohammed Al-Ghazaly pamoja na Mratibu wa Programu hiyo Bw. Stephano D. Mgani.

Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 06 Novemba, 2024, na kulenga ufuatiliaji wa utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), ambayo pia ni Programu inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu.

Aidha, Wataalamu hao wameeleza kufurahishwa na utekelezaji wa programu tangu kuanzishwa kwake mwaka 2022 anbapo umechangia ongezeko la uzalishaji wa mbegu na uwekaji wa miundombinu katika mashamba ya mbegu ili kuwa na kilimo chenye tija kwa wakulima.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

NYONGEZA NA. 1 YA MWONGOZO NA. 2 WA USIMAMIZI NA UDHIBITI UBORA WA KOROSHO GHAFI KWA MWAKA 2023/2024

Peter Luambano

MKUU WA MKOA WA MTWARA AZINDUA MINADA YA KOROSHO KWA MSIMU WA 2022/2023 LEO TAREHE 21 OKTOBA KWA VYAMA VIKUU VIWILI TANECU NA MAMCU MKOANI MTWARA.

Peter Luambano

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA BODI YA KOROSHO TANZANIA

Peter Luambano