Mei 1, 2025 01:09
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

SHILINGI BILIONI 743.57 /= ZAPATIKANA MAUZO YA KOROSHO MSIMU WA 2024/2025

Wakati minada ya korosho katika msimu wa 2024/2025 ikiendelea, Mkurugezi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari novemba 4, 2024 amesema kuwa jumla ya Tsh bilioni 743.57/= zimepatikana Katika wiki nne za minada ya korosho.

Huku wakulima zaidi ya asilimia 90 wakiwa wamelipwa fedha zao hadi sasa, bei za korosho katika minada inayoendelea ni nzuri na sababu kubwa zikitajwa kuwa ni usimamizi mzuri wa Vyama Vikuu vya Ushirika, Bodi ya Korosho Tanzania na ubora wa korosho zinazouzwa.

Changamoto mbalimbali ikiwamo ya usafiri na malipo zimeendelea kushughulikiwa kwa ukaribu ambapo magari yameongezwa ili kubeba korosho kutoka vyama vya msingi kuelekea ghala kuu na wakulimwa wenye changamoto ya malipo wamekumbushwa kuwasiliana na viongozi wa AMCOS au Bodi ya Korosho Tanzania kwa utatuzi zaidi.

“Tayari tumeongea na Vyama vya Ushirika kuhakikisha wanafuatilia hizo changamoto ndogo ndogo na kwenda kwenye benki husika ili akaunti zote ambazo zina changamoto wakulima wapatiwe stahiki zao.” Ndg. Alfred

Vilevile Mkurugenzi mkuu amewatoa wasiwasi wakulima kuwa zoezi hilo litalishugulikiwa ndani ya wiki hii  na malipo yote yaliyo kwama Katika minada iliyopita, viongozi watahakikisha wakulima wanapatiwa haraka iwezekanavyo.

Related posts

MAAFISA KILIMO WA BBT KOROSHO WAENDELEA NA MAFUNZO YA VITENDO

Amani Ngoleligwe

KITABU CHA KILIMO BORA CHA KOROSHO

Amani Ngoleligwe

KIKAO CHA NNE CHA BODI YA WAKURUGENZI BODI YA KOROSHO

Fesam