Septemba 18, 2025 12:06
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MIKUTANO MUHIMU KUHUSU KILIMO-MAREKANI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki katika mijadala muhimu ya kimataifa kuhusu kilimo barani Afrika ambayo ni Africa Agriculture Dialogue (AAD) ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB); na mjadala wa Kimataifa wa Norman E. Borlaug, ulioandaliwa na Taasisi ya World Food Foundation katika mji wa Des Moines, jimbo la Iowa, Marekani, mnamo Oktoba 30, 2024.

Katika hotuba zake, Mhe. Rais Dkt. Samia ameeleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Tanzania ili kuwa mzalishaji mkubwa wa chakula kwa ajili ya kujitosheleza kama Taifa na kuuza Chakula cha ziada kibiashara (feed ourselves, feed others commercially). Aidha, Mhe. Rais Dkt. Samia alibainisha jinsi nchi inavyoimarisha mifumo ya uzalishaji wa chakula kwa kutumia teknolojia za kisasa ili kufikia malengo hayo kama Taifa.


Mikutano hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb); Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo wa Zanzibar, Mhe. Shamata Shaame Khamis (Mb); na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli.

Related posts

BODI YA KOROSHO YATOA MASHINE ZA UBANGUAJI KOROSHO

Amani Ngoleligwe

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred Pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI)-Naliendele Dkt Fortunus Kapinga wamepokea ujumbe wa wageni kutoka Nchini Benin leo tarehe 3 Octoba 2022.

Peter Luambano

MAONESHO YA NANENANE 2022-MBEYA

Fesam