Disemba 31, 2025 02:46
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

LINDI MWAMBAO WAUZA TANI 5,106 KWA BEI YA JUU SH. 2,460 KUPITIA MFUMO WA TMX

Jumla ya tani 5,106 za korosho ghafi zimeuzwa kupitia mfumo wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) katika mnada wa kwanza wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao mkoani Lindi, kwa bei ya juu ya shilingi 2,460 na bei ya chini ya shilingi 2,310 kwa kilo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred amesema mnada huo umefanyika kwa mafanikio makubwa, huku akibainisha kuwa mfumo wa TMX ni mfumo wa uwazi na ushindani katika biashara ya korosho.

Aidha Mkurugenzi ametoa wito kwa wakulima wote kuendelea kuzingatia ubora wa korosho zao kwa kuzikausha vizuri, kwani soko zuri hutegemea ubora wa zao.

Mnada huu umefanyika novemba 9, 2025 ukiwa ni wa pili tangu kuanza kwa minada ya zao la korosho nchini katika msimu wa 2025/2026. Mnada wa kwanza ulifanyika Novemba 8,2025. kupitia Chama Kikuu cha Ushirika Cha Tandahimba na Newala (TANECU).

Related posts

MWONGOZO NA. 2 WA USIMAMIZI NA UDHIBITI UBORA WA KOROSHO GHAFI WA MWAKA 2023/2024 TOLE0 LA 6

Peter Luambano

TAARIFA FUPI YA MINADA YA KOROSHO ILIYOFANYIKA TAREHE 20 OKTOBA. 2023 A.TANECU LTD KATIKA UKUMBI WA TANDAHIMBA DC

Peter Luambano

TANGAZO KWA WADAU WOTE WA TASNIA YA KOROSHO NCHINI. NOV 11-2024

Amani Ngoleligwe