Mei 12, 2026 07:05
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

LINDI MWAMBAO WAUZA TANI 5,106 KWA BEI YA JUU SH. 2,460 KUPITIA MFUMO WA TMX

Jumla ya tani 5,106 za korosho ghafi zimeuzwa kupitia mfumo wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) katika mnada wa kwanza wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao mkoani Lindi, kwa bei ya juu ya shilingi 2,460 na bei ya chini ya shilingi 2,310 kwa kilo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred amesema mnada huo umefanyika kwa mafanikio makubwa, huku akibainisha kuwa mfumo wa TMX ni mfumo wa uwazi na ushindani katika biashara ya korosho.

Aidha Mkurugenzi ametoa wito kwa wakulima wote kuendelea kuzingatia ubora wa korosho zao kwa kuzikausha vizuri, kwani soko zuri hutegemea ubora wa zao.

Mnada huu umefanyika novemba 9, 2025 ukiwa ni wa pili tangu kuanza kwa minada ya zao la korosho nchini katika msimu wa 2025/2026. Mnada wa kwanza ulifanyika Novemba 8,2025. kupitia Chama Kikuu cha Ushirika Cha Tandahimba na Newala (TANECU).

Related posts

TANECU WAUZA KOROSHO KWA BEI YA JUU TSH. 3760/= NA BEI YA CHINI TSH.3540/=, UBORA WASISITIZWA.

Amani Ngoleligwe

MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA UGAWAJI WA PEMBEJEO KWA MSIMU WA 2023/2024

Peter Luambano

MELI YA KWANZA KATI YA NNE ZINAZOTARAJIA KUBEBA TANI 40,000 ZA PEMBEJEO ZA ZAO LA KOROSHO YAWASILI BANDARI YA MTWARA

Amani Ngoleligwe