Juni 18, 2026 12:29
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KATIBU MKUU MWELI AKUTANA NA BALOZI WA ITALIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Italia hapa nchini, Mhe. Giuseppe Sean Coppola jijini Dodoma tarehe 5 Novemba 2024.

Viongozi hao wamekutana kwa ajili ya utambulisho na kuzungumza kuhusu kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Kilimo hususan katika masuala ya utafiti ili kuchochea ugunduzi wa teknolojia mbalimbali kwenye Sekta hiyo.

Mhe. Balozi Coppola ameelezea kuwa Italia ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha mnyororo wa thamani wa zao la kahawa.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Mweli alimshukuru Mhe. Balozi Coppola na kueleza kuwa Wizara ya Kilimo ina fursa za uwekezaji hivyo alihamasisha na kukaribisha wawekezaji kutoka nchini Italia kuwekeza katika Sekta ya Kilimo nchini; hususan katika maeneo ya uzalishaji wa zana za kilimo kama vile matrekta.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

MELI YA KWANZA KATI YA NNE ZINAZOTARAJIA KUBEBA TANI 40,000 ZA PEMBEJEO ZA ZAO LA KOROSHO YAWASILI BANDARI YA MTWARA

Amani Ngoleligwe

MWONGOZO NA.3 WA UNUNUZI WA KOROSHO KWENYE SOKO LA AWALI KWA AJILI YA WABANGUAJI WA NDANI MSIMU WA 2025/2026

Amani Ngoleligwe

UZINDUZI WA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Fesam