Agosti 21, 2025 07:22
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KATIBU MKUU MWELI AKUTANA NA BALOZI WA ITALIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Italia hapa nchini, Mhe. Giuseppe Sean Coppola jijini Dodoma tarehe 5 Novemba 2024.

Viongozi hao wamekutana kwa ajili ya utambulisho na kuzungumza kuhusu kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Kilimo hususan katika masuala ya utafiti ili kuchochea ugunduzi wa teknolojia mbalimbali kwenye Sekta hiyo.

Mhe. Balozi Coppola ameelezea kuwa Italia ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha mnyororo wa thamani wa zao la kahawa.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Mweli alimshukuru Mhe. Balozi Coppola na kueleza kuwa Wizara ya Kilimo ina fursa za uwekezaji hivyo alihamasisha na kukaribisha wawekezaji kutoka nchini Italia kuwekeza katika Sekta ya Kilimo nchini; hususan katika maeneo ya uzalishaji wa zana za kilimo kama vile matrekta.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

SHILINGI BILIONI 743.57 /= ZAPATIKANA MAUZO YA KOROSHO MSIMU WA 2024/2025

Amani Ngoleligwe

Mh DUNSTAN KYOBA AFANYA ZIARA YA KUSHITUKIZA BODI YA KOROSHO.

Peter Luambano

BODI YA KOROSHO YAPOKEA TANI 3,680 YA SULPHUR KUPITIA BANDARI YA MTWARA

Peter Luambano