Juni 17, 2025 08:53
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

DKT. SERERA AONGOZA KIKAO NOVEMBA 13-2024

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (Ushirika na Umwagiliaji), Dkt. Suleiman Serera ameongoza kikao cha pamoja kati ya Wizara na Washiriki wa Maendeleo tarehe 13 Novemba 2024 kujadili namna Wizara inavyotekeleza majukumu yake yanayohusu usalama wa chakula, mfumo wa usajili wa wakulima pamoja na kilimo kinachokabiliana na mabadiliko ya tabia nchi (Climate Smart Agriculture) kwa ajili ya maoni yatakayotumika katika kuandaa Mpango wa Awamu ya Tatu wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN III) utakaotekelezwa na TASAF.

Timu hiyo imehusisha wataalamu mbalimbali kutoka Benki ya Dunia, Ubalozi wa Norway, Ubalozi wa Uswizi, Ubalozi wa Uingereza, Irish Aid, Jumuiya ya Madola, Umoja wa Ulaya, WFP na UNISEF wakiongozwa na Claudia Zambra kutoka Benki ya Dunia.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

BASHE:  BENKI YA USHIRIKA TANZANIA (COOP BANK TANZANIA) KUANZA NA MTAJI WA BILLIONI 55

Amani Ngoleligwe

MELI YA KWANZA KATI YA NNE ZINAZOTARAJIA KUBEBA TANI 40,000 ZA PEMBEJEO ZA ZAO LA KOROSHO YAWASILI BANDARI YA MTWARA

Amani Ngoleligwe

BODI YA KOROSHO TANZANIA (CBT) YAWATAKA WAKULIMA KUENDELEA KUDUMISHA UBORA WA KOROSHO.

Amani Ngoleligwe