Juni 16, 2025 03:38
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

DKT. KIRUSWA ATEMBELEA BANDA LA MAONESHO CBT NA KUPONGEZA JUHUDI ZA RAIS DKT. SAMIA

Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wakulima wa korosho ikiwa ni pamoja na kuwapatia pembejeo za ruzuku na kuwa na utashi wa kisiasa katika kuendeleza Sekta ya Kilimo nchini.

Pia Dkt. Kiruswa ameipongeza Bodi ya Korosho Tanzania kwa kazi nzuri wanazozifanya ikiwa ni pamoja na kuwasimamia wakulima wa zao la korosho wa Kanda ya kusini na mikoa mingine nchini.

Ameyasema hayo leo juni 13, 2024 alipotembelea banda la Bodi ya Korosho wakati wa Maonesho ya Madini na Uwekezaji wilayani Ruangwa mkoani Lindi. Maonesho hayo yameanza rasmi tarehe 11 na yanatarajiwa kufikia tamati tarehe 14 juni 2025.

Related posts

TAARIFA KWA WADAU WOTE WA TASNIA YA KOROSHO NCHINI/ NOTICE TO ALL STAKEHOLDERS IN THE CASHEWNUT INDUSTRY

Peter Luambano

WAKULIMA MNOLELA: TANGU TUANZE KUPOKEA PEMBEJEO ZA RUZUKU MAMBO YANAKWENDA VIZURI SANA

Amani Ngoleligwe

WAKULIMA WA KOROSHO KUENDELEA KUNEEMEKA NA PEMBEJEO ZA RUZUKU YA SERIKALI.

Peter Luambano