Aprili 15, 2026 02:25
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BODI YA KOROSHO TANZANIA YATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA HUSSEIN BASHE (MB)

Bodi ya Korosho Tanzania yatekeleza agizo la Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe (MB) kwa kutoa vitabu vya kusajili wakulima wa korosho Jimbo la Mtama Mkoa wa Lindi.  Maafisa wa Bodi wametoa mafunzo kwa Maafisa Ugani wa Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Mtama namna ya kujaza taarifa za wakulima ikiwa na lengo na mwendelezo wa maboresho ya taarifa za awali zilizopo kwenye mfumo wa kidigitali wa usajili wa wakulima(FRS).
Vitabu hivi vimetolewa kwa lengo la kupata taarifa za uhakiki wa usajili uliofanyika awali wa  taarifa za wakulima wa korosho kwani taarifa zao ziko kwenye  mfumo wa FRS uliotolewa na Wizara ya Kilimo.

Related posts

TANI 180,342 ZA KOROSHO ZAUZWA NDANI YA WIKI TATU MSIMU WA 2024/2025.

Amani Ngoleligwe

MWONGOZO Na.2 WA USIMAMIZI NA UDHIBITI UBORA WA KOROSHO GHAFI WWA MWAKA 2025/2026.pdf

Amani Ngoleligwe

TANGAZO KWA WADAU WA TASNIA YA KOROSHO

Amani Ngoleligwe