Mei 24, 2025 12:20
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BODI YA KOROSHO NA TARI WAFANYA KIKAO CHA PAMOJA

Bodi ya Korosho (CBT) na kituo cha Utafiti wa Kilimo Tanzania-Naliendele (TARI) wamekutana na kufanya kikao cha pamoja katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Korosho Mjini Mtwara tarehe 20 Machi, 2023.

Lengo kuu la kikao hicho ni kuimarisha mahusiano zaidi ya kiutendaji katika uendelezaji wa tasnia ya Korosho Tanzania,ikumbukwe kuwa taasisi hizi zote zipo chini ya wizara ya Kilimo na zinamajukumu tofauti ikiwa ni kusimamia,kuendeleza na kukuza tasnia ya Korosho.

Kupitia kikao hiki, mwenyekiti wa kikao ambae pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI-Nalendele Dkt. Fortunus A.Kapinga; ameelezea namna TARI inavyofanya kazi lakini pia mchango wa TARI katika uendelezaji wa zao la Korosho Tanzania.

Dkt.Kapinga amesisitiza zaidi ushirikiano baina ya watumishi wa TARI na Bodi ya Korosho katika utendaji kazi ukizingatia taasisi zote mbili zinamalengo sawa kwenye kuendeleza,kusimamia na kukuza zao la Korosho.

Kupitia kikao hicho,Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania ambae pia ni Mwenyekiti mwenza wa kikao Ndg. Francis Alfred,ameiomba TARI kusaidia tasnia ya Korosho hasa katika kufanya tafiti nyingi ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazolikabili zao la Korosho.

Related posts

Wajumbe wakiwa kwenye Mkutano wa kimataifa wa korosho uliofanyika Tanzania katika ukumbi wa Mikutano ya kimataifa wa Julius Nyerere

Peter Luambano

BODI YA KOROSHO KUTOA MAFUNZO KWA WAKULIMA WA KOROSHO WILAYA YA BIHARAMULO-KAGERA

Peter Luambano

MKUTANO MKUU WA WADAU WA TASNIA YA KOROSHO 2024

Peter Luambano