Agosti 21, 2025 09:03
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA RUFIJI LATEMBELEA BODI YA KOROSHO MTWARA.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji , wameitembelea Bodi ya Korosho Tanzania kwa ajili ya kujifunza shughuli mbali mbali zinazofanywa ikiwa Pamoja na Masuala ya Pembejeo, Kilimo , Ubanguaji na Masoko.

Katika ziara hiyo Baraza la Madiwani waliweza kupata taarifa mbalimbali zinzohusu zao la Korosho Pamoja na kujifunza namna bora ya kuongeza thamani katika zao hilo, hata hivyo Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bwana Francis Alfred aliwaomba Waheshimiwa Madiwani kuwa Bodi imeomba eneo katika wilaya yao ya Rufiji jumla ya Hekali 5,000 ambapo ndani ya hekali hizo kutakuwa na Mashamba Makubwa ya Pamoja kwa ajili ya Vijana wa Rufiji, Wafanyakazi wa Bodi ya Korosho Tanzania na Makatibu Wakuu wa Wizara zote, hivyo iwapo Bodi itapatiwa eneo hilo basi Rufiji itakuwa ni moja ya sehemu yenye mashamba makubwa ya mfano Tanzania.

Related posts

KATIBU MKUU MWELI AKUTANA NA BALOZI WA ITALIA

Amani Ngoleligwe

MAONESHO YA NANENANE 2022-MBEYA

Fesam

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred Pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI)-Naliendele Dkt Fortunus Kapinga wamepokea ujumbe wa wageni kutoka Nchini Benin leo tarehe 3 Octoba 2022.

Peter Luambano