Mei 1, 2025 10:03
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

SILINDE ASHIRIKI COP29 NCHINI AZERBAIJAN.

Mhe.David Silinde (Mb), Naibu Waziri wa Kilimo akiambatana na Dkt. Hussein Omary, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula) pamoja na wataalam wengine wa Wizara ya Kilimo wameshiriki katika Mkutano wa 29 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP29) unaofanyika katika mji wa Baku, nchini Azerbaijan.

Katika Mkutano huo, Wizara imeshiriki katika majadiliano na Mwakilishi wa Mfuko wa Ufadhili wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) na kujadili masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na namna ya kuwasilisha miradi ya vipaumbele ya pamoja kwa mfuko huo kwa mwaka 2025.

CHANZO: Wizara ya Kilimo

Related posts

UHUISHAJI TAARIFA ZA WAKULIMA WA KOROSHO WAENDELEA KWA MAFANIKIO KATIKA KATA YA NYANGAO MKOANI LINDI

Amani Ngoleligwe

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Francis Alfred, akizungumza na Wakulima wakati wa ufunguzi wa mnada wa kwanza wa ununuzi wa Korosho Msimu 2023/2024 katika Kijiji cha Mburusa Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Octoba 20,2023

Peter Luambano

TANZANIA YAPATA SOKO JIPYA LA KOROSHO BARANI ULAYA

Peter Luambano