Aprili 20, 2025 12:58
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

MKUU WA MKOA WA MTWARA AFUNGA MAFUNZO YA UDHIBTI UBORA

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanal Ahmed Abbasi amefunga mafunzo ya siku tano ya udhibiti ubora wa korosho kwa washiriki 120 yaliyoratibiwa na Bodi ya korosho Tanzania na kufikia tamati tarehe 23 septemba, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa chuo mafunzo ya kilimo MATI kilichopo kata ya Naliendele Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Akizungumza katika hafla hiyo,kanal Ahmed amesema Serikali haitosita kuwachukulia hatua kali wale wote watakaojihusisha na vitendo viovu vya kuihujumu korosho kwa msimu huu unaotarajia kuanza Oktoba 14, 2022.

Aidha,ametoa wito wa kuongeza mikorosho mipya ili kuongeza tija katika uzalishaji wa korosho na kufikia malengo ya wizara ya kilimo(CBT-Mtwara HQ).

CHUO CHA KILIMO MATI-MANISPAA YA MTWARA MIKINDANI

Related posts

Wajumbe wakiwa kwenye Mkutano wa kimataifa wa korosho uliofanyika Tanzania katika ukumbi wa Mikutano ya kimataifa wa Julius Nyerere

Peter Luambano

TICC CONFERENCE ANNOUNCEMENT AND CALL FOR PRESENTATIONS

Peter Luambano

KATIBU MKUU MWELI AKUTANA NA BALOZI WA ITALIA

Amani Ngoleligwe