Mei 14, 2026 01:04
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA RUFIJI LATEMBELEA BODI YA KOROSHO MTWARA.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji , wameitembelea Bodi ya Korosho Tanzania kwa ajili ya kujifunza shughuli mbali mbali zinazofanywa ikiwa Pamoja na Masuala ya Pembejeo, Kilimo , Ubanguaji na Masoko.

Katika ziara hiyo Baraza la Madiwani waliweza kupata taarifa mbalimbali zinzohusu zao la Korosho Pamoja na kujifunza namna bora ya kuongeza thamani katika zao hilo, hata hivyo Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bwana Francis Alfred aliwaomba Waheshimiwa Madiwani kuwa Bodi imeomba eneo katika wilaya yao ya Rufiji jumla ya Hekali 5,000 ambapo ndani ya hekali hizo kutakuwa na Mashamba Makubwa ya Pamoja kwa ajili ya Vijana wa Rufiji, Wafanyakazi wa Bodi ya Korosho Tanzania na Makatibu Wakuu wa Wizara zote, hivyo iwapo Bodi itapatiwa eneo hilo basi Rufiji itakuwa ni moja ya sehemu yenye mashamba makubwa ya mfano Tanzania.

Related posts

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA BODI YA KOROSHO TANZANIA

Peter Luambano

TANGAZO KUHUSU USAJILI WA WAENDESHA GHALA KATIKA ZAO LA KOROSHO

Amani Ngoleligwe

MWONGOZO NA. 2 WA USIMAMIZI NA UDHIBITI UBORA WA KOROSHO GHAFI WA MWAKA 2023/2024 TOLE0 LA 6

Peter Luambano