Machi 11, 2026 12:32
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

WAZIRI JAFO AHITIMISHA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KUSINI

Waziri wa Viwanda na Biashara nchini Mhe. Dkt. Suleiman Jafo amehitimisha rasmi maonesho ya sikukuu ya wakulima (NANENANE) kanda ya kusini – Ngongo mkoani Lindi.

Dkt. Jafo amepongeza mfumo wa stakabadhi ghalani unaotumiwa na wakulima, mfumo ambao ni wenye tija na unalenga kumnufaisha mkulima na jamii kwa ujumla ikiwamo kutoa ajira.

Aidha wizara ya kilimo imeshika nafasi ya kwanza kwenye maonesho haya kanda ya kusini na kwa upande wa mamlaka za udhibiti, Bodi ya Korosho Tanzania imeibuka mshindi wa kwanza kwenye maonesho haya ukanda wa kusini.

Kwa ukanda wa kusini maonesho haya yalifunguliwa rasmi na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala Agosti 1-2025 na yamehitimishwa rasmi na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Jafo Agosti 8-2025.

Related posts

MAAFISA KILIMO WA BBT KOROSHO WAENDELEA NA MAFUNZO YA VITENDO

Amani Ngoleligwe

FURSA ZA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA

Peter Luambano

WAKULIMA WA KOROSHO KUENDELEA KUNEEMEKA NA PEMBEJEO ZA RUZUKU YA SERIKALI.

Peter Luambano