Aprili 14, 2026 02:11
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

TIMU YA WAKAGUZI YAKAMILISHA KAZI CBT

Timu ya wakaguzi kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma imekamililisha zoezi la ukaguzi katika taasisi ya Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) kwa jumla ya hoja kumi (10, zoezi ambalo limefanyika kwa muda wa siku nne kuanzia septemba 19 hadi 22, 2025.

Hoja zilizokaguliwa ni pamoja na Ajira mpya, Upandishwaji vyeo, Mafunzo na maendeleo ya watumishi, Nidhamu, Uzingatiaji wa maadili, Anuai za Jamii, Ufuatiliaji wa usalama na afya mahali pa kazi, Usimamizi wa taarifa, utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka, fidia ya magonjwa sugu, na katika hoja hizo, CBT imepongezwa kwa kufanya vema upande wa nidhamu.

Eneo lingine lililofanywa vizuri na CBT ni pamoja na likizo ya mwaka kwa watumishi ambapo watumishi wanaostahili kupata likizo, walipata na walirejea kwa wakati kwenye majumu yao, na taarifa zote kuhusu likizo hufanyiika katika mfumo maalumu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu ndg. Revelian S. Ngaiza, ameshukuru juu ya zoezi hilo na kupokea maoni yaliyotokana na ukaguzi huo pamoja na kuahidi kuyafanyia kazi.

Timu ya wakaguzi hao, imeongozwa na bw. Muhidin A. Muro sambamba na   bi. Hajra H. Mabrouk, bw. Gift S. Lyimo na bw. Florence Mboya.

Related posts

TANECU WAUZA KOROSHO KWA BEI YA JUU TSH. 3760/= NA BEI YA CHINI TSH.3540/=, UBORA WASISITIZWA.

Amani Ngoleligwe

BODI YA KOROSHO TANZANIA YASHIRIKI WIKI YA UWEKEZAJI NA BIASHARA MKOANI PWANI

Peter Luambano

DKT SERERA AZINDUA MRADI WA GROWING TOGETHER

Amani Ngoleligwe