Aprili 30, 2025 08:17
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KOROSHO QUEENS YAPATA UFADHILI WA VIFAA VYA MICHEZO

Bodi ya korosho imekabidhi vifaa vya michezo ikiwemo Mipira,Viatu na Sare kwa timu ya mpira ya KOROSHO QUEENS siku ya tarehe 11/05/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Korosho Mtwara,makabidhiano hayo yamefanywa kati ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi Ndug. Gerald Rogathe na uongozi wa KOROSHO QUEENS wakiongozwa na Meneja wa Timu hiyo Ndug. Hussein Omary Kibombwe.

Vifaa hivyo vimetolewa na Bodi ya korosho kwa kuzingatia ombi la ufadhili lililoletwa na KOROSHO QUEENS,aidha kwa kuzingatia umuhimu wa michezo,Bodi imetekeleza ombi hilo kama walivyoleta na pia imewaomba wadau wengine wa michezo kuchangia na kutoa chochote ili kuendeleza ndoto ya timu hii iliyopo mjini Mtwara.

Related posts

WIZARA YA KILIMO YAKARIBISHA WAWEKEZAJI KONGANI LA VIWANDA MARANJE-MTWARA

Amani Ngoleligwe

Wajumbe wakiwa kwenye Mkutano wa kimataifa wa korosho uliofanyika Tanzania katika ukumbi wa Mikutano ya kimataifa wa Julius Nyerere

Peter Luambano

NAIBU WAZIRI SILINDE AZINDUA MIRADI KATIKA SEKTA YA KILIMO

Amani Ngoleligwe