Oktoba 15, 2025 03:10
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

KIKAO CHA SITA CHA BODI YA WAKURUGENZI WA BODI YA KOROSHO TANZANIA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Brig. Gen. (Mstaafu) Aloyce Damian Mwanjile ndc ameongoza kikao cha Bodi ya Wakurugenzi tarehe 19 Oktoba 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Korosho Tanzania kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu Mtwara
Menejimenti imewasilisha taarifa ya utekelezaji wa maazigo ya kikao kilichopita, taarifa ya utekelezaji wa robo ya kwanza, mipango ya utekelezaji kwa robo ya pili ya mwaka 2022/2023. Pia Bodi imepitia utekelezaji wa maagizo ya viongozi yaliyotolewa huko nyuma ikiwa ni pamoja na maandalizi ya msimu wa mauzo ya korosho ya mwaka 2022/2023.
Akiongea katika kikao hicho, Mwenyekiti amesisitiza kuongeza ufanisi katika kutekeleza shughuli zilizopangwa na kupitishwa ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa.
Sambamba na hayo, Mwenyekiti ameipongeza Menejimenti kwa uwajibikaji mzuri katika kutimiza majukumu yao ya kazi.

Related posts

MKUU WA MKOA WA MTWARA AZINDUA MINADA YA KOROSHO KWA MSIMU WA 2022/2023 LEO TAREHE 21 OKTOBA KWA VYAMA VIKUU VIWILI TANECU NA MAMCU MKOANI MTWARA.

Peter Luambano

MWONGOZO NA. 2 WA USIMAMIZI NA UDHIBITI UBORA WA KOROSHO GHAFI WA MWAKA 2023/2024 TOLE0 LA 6

Peter Luambano

WADAU WA KOROSHO WAKUTANA KUPITIA MIONGOZO KWA MSIMU WA 2025/2026

Amani Ngoleligwe