Januari 31, 2026 07:53
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BODI YA KOROSHO YATOA JEZI ZA MICHEZO KWA JESHI LA ZIMAMOTO TANZANIA

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg.Reuben Putaputa amekabidhi Jezi za Mpira wa Miguu pamoja na Mipira kwa Jeshi la Zimamoto Tanzania Mkoani Mtwara.

Makabidhiano haya yamefanyika katika Ofisi za Bodi ya Korosho Makao Makuu Mtwara tarehe 27 Machi 2023, aidha kwa kutambua mchango wa jeshi hili katika kulinda usalama na majanga eneo la kazi,Bodi ya Korosho imeona ni vyema kutekeleza zoezi hili ili kuwajengea Afya itokanayo na Michezo lakini pia kuboresha mahusiano na mshikamano katika kujenga Taifa letu.

Akipokea jezi hizo kwa niaba ya Jeshi la Zimamoto Tanzania, Inspekta Elizabeth Mpondela ameishukuru Bodi na kuahidi kuendeleza ushirikiano katika kila jambo ili kuhakisha usalama sehemu za kazi inakua ni kipaumbele.

Related posts

KANALI SAWALA: MAFUNZO YA UMAHIRI KWENYE MNYORORO WA THAMANI WA ZAO LA KOROSHO KULETA TIJA KWA WASHIRIKI

Amani Ngoleligwe

BODI YA KOROSHO TANZANIA YASHIRIKI WIKI YA UWEKEZAJI NA BIASHARA MKOANI PWANI

Peter Luambano

WADAU WAASWA KUZINGATIA UBORA KATIKA ZAO LA KOROSHO

Peter Luambano