Januari 16, 2026 06:05
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKitelezi

WAZIRI WA KILIMO MHE.HUSSEIN BASHE (MB) ASISITIZA ZOEZI LA USAJILI WA WAKULIMA WA KOROSHO NCHINI

Akizungumza katika kikao cha tathmini kilichofanyika Jijini Dodoma tarehe 24 April 2023, Mhe. Bashe amesisitiza usajili wa Wakulima kupitia kanzi data ya Wakulima Nchi nzima ikiwa ni moja ya utekelezaji wa Agenda ya 10/30 ya Kilimo.

Katika kukazia hili,Mhe. Bashe ameiagiza Bodi ya Korosho Nchini kusimamia zoezi hili kikamilifu na kuhakikisha kila Mkulima anaingia kwenye kanzi data,aidha ameongeza kwa kusema, kwasasa hakuna Mkulima wa Korosho atakaepata Pembejeo iwapo hajaingia kwenye kanzi data ya Kilimo.

“Hii itaondoa malalamiko katika zoezi la usambazaji na ugawaji wa ruzuku ya Pembejeo lakini pia usajili huuu utaisaidia Serikali katika jitihada zake za kufanya makadirio ya kuwawezesha Wakulima wa Korosho ili kuongeza uzalishaji na tija katika zao la Korosho”(Mhe.Hussein Bashe).

Related posts

MKUTANO MKUU WA WADAU WA TASNIA YA KOROSHO 2024

Peter Luambano

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MIKUTANO MUHIMU KUHUSU KILIMO-MAREKANI

Amani Ngoleligwe

BODI YA KOROSHO NA MWENDELEZO WA UBORESHAJI WA KANZI DATA YA WAKULIMA WA KOROSHO NCHINI

Peter Luambano