Juni 20, 2026 05:33
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

TARI WAJIANDAA KUPOKEA MEDALI KOROSHO MARATHON

Ni Wafanyakazi wa Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Naliendele wakiwa katika picha ya pamoja oktoba 22/2024 mara baada ya kupata jezi na vifaa vingine tayari kwa ajili ya Korosho Marathon huku wakiwa wamejipanga kupokea medali katika mashindano hayo.

Unaweza kupata vifaa hivyo katika eneo la Bima Mtwara mjini na usajili unaendelea hadi tarehe 24 oktoba huku kilele chake kikiwa jumamosi ya tarehe 26 oktoba 2024 huko Milleneum Beach na mgeni rasmi atakuwa naibu waziri wa sanaa utamaduni na michezo Mhe. Khamis Mwinjuma.

Hii ni awamu ya tatu ya Korosho Marathon, ambapo kwa mara ya kwanza ilizinduliwa mwaka 2022 ikiwa na watu wapatao 450 waliojisajili na mwaka 2023 waliojisajili walikuwa 1763 na mwaka huu zoezi la kujisajili linaendelea hadi tarehe 24 oktoba.

Related posts

MKUTANO WA 19 WA ACA WA MWAKA NA MAONESHO YA BIDHAA YA KOROSHO NOV 18 – 21 NOV 2025

Amani Ngoleligwe

Bodi ya Korosho yawaonya wafanyabiashara wanaozitorosha Korosho nje ya nchi

Peter Luambano

RATIBA YA MINADA MSIMU WA 2025/2026

Amani Ngoleligwe