Januari 24, 2026 11:26
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

MKULIMA WA KOROSHO KULIPWA SIKU 7 BAADA YA MNADA

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred ametoa ufafanuzi juu ya malipo ya wakulima wa Korosho nchini katika kuelekea msimu huu wa mwaka 2024/2025.

Ndg. Alfred amesema Wanunuzi wa Korosho watalipa fedha kwa vyama vikuu vya ushirika ndani ya siku 5 baada ya mnada kufanyika na Vyama vikuu vinatakiwa kukamilisha malipo hayo kwa wakulima ndani ya saa 48 ambayo ni sawa na siku 2 ili wakulima wapate fedha zao za mauzo, hivyo mkulima atapata malipo yake siku 7 baada ya mnada kufanyika.

Mnada wa kwanza wa Korosho nchini kwa msimu wa mwaka 2024-2025 unatarajiwa kufanyika Oktoba 11,2024 kwa kuanzia na chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU.

Related posts

KOROSHO MARATHON KUENDELEA KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA TASNIA YA KOROSHO

Amani Ngoleligwe

WAKULIMA MNOLELA: TANGU TUANZE KUPOKEA PEMBEJEO ZA RUZUKU MAMBO YANAKWENDA VIZURI SANA

Amani Ngoleligwe

BODI YA KOROSHO YATOA MASHINE ZA UBANGUAJI KOROSHO

Amani Ngoleligwe