Febuari 5, 2026 02:19
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

MKULIMA WA KOROSHO KULIPWA SIKU 7 BAADA YA MNADA

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred ametoa ufafanuzi juu ya malipo ya wakulima wa Korosho nchini katika kuelekea msimu huu wa mwaka 2024/2025.

Ndg. Alfred amesema Wanunuzi wa Korosho watalipa fedha kwa vyama vikuu vya ushirika ndani ya siku 5 baada ya mnada kufanyika na Vyama vikuu vinatakiwa kukamilisha malipo hayo kwa wakulima ndani ya saa 48 ambayo ni sawa na siku 2 ili wakulima wapate fedha zao za mauzo, hivyo mkulima atapata malipo yake siku 7 baada ya mnada kufanyika.

Mnada wa kwanza wa Korosho nchini kwa msimu wa mwaka 2024-2025 unatarajiwa kufanyika Oktoba 11,2024 kwa kuanzia na chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU.

Related posts

VIONGOZI CBT WAKUTANA NA WAGENI KUTOKA UHOLANZI KUJADILI UONGEZAJI THAMANI ZAO LA KOROSHO

Amani Ngoleligwe

KIKAO CHA SITA CHA BODI YA WAKURUGENZI WA BODI YA KOROSHO TANZANIA

Peter Luambano

KUSITISHWA KWA KONGAMANO NA MAONESHO YA 19 YA MWAKA YA AFRICAN CASHEW ALLIANCE (ACA)

Amani Ngoleligwe