Disemba 7, 2025 12:06
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

MKULIMA WA KOROSHO KULIPWA SIKU 7 BAADA YA MNADA

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg. Francis Alfred ametoa ufafanuzi juu ya malipo ya wakulima wa Korosho nchini katika kuelekea msimu huu wa mwaka 2024/2025.

Ndg. Alfred amesema Wanunuzi wa Korosho watalipa fedha kwa vyama vikuu vya ushirika ndani ya siku 5 baada ya mnada kufanyika na Vyama vikuu vinatakiwa kukamilisha malipo hayo kwa wakulima ndani ya saa 48 ambayo ni sawa na siku 2 ili wakulima wapate fedha zao za mauzo, hivyo mkulima atapata malipo yake siku 7 baada ya mnada kufanyika.

Mnada wa kwanza wa Korosho nchini kwa msimu wa mwaka 2024-2025 unatarajiwa kufanyika Oktoba 11,2024 kwa kuanzia na chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU.

Related posts

HALI YA SOKO LA KOROSHO GHAFI KWA MWAKA 2022/2023

Peter Luambano

NYONGEZA NA. 1 YA MWONGOZO NA. 2 WA USIMAMIZI NA UDHIBITI UBORA WA KOROSHO GHAFI KWA MWAKA 2023/2024

Peter Luambano

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Francis Alfred, akizungumza na Wakulima wakati wa ufunguzi wa mnada wa kwanza wa ununuzi wa Korosho Msimu 2023/2024 katika Kijiji cha Mburusa Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Octoba 20,2023

Peter Luambano