Juni 17, 2025 02:57
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BODI YA KOROSHO TANZANIA YATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA HUSSEIN BASHE (MB)

Bodi ya Korosho Tanzania yatekeleza agizo la Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe (MB) kwa kutoa vitabu vya kusajili wakulima wa korosho Jimbo la Mtama Mkoa wa Lindi.  Maafisa wa Bodi wametoa mafunzo kwa Maafisa Ugani wa Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Mtama namna ya kujaza taarifa za wakulima ikiwa na lengo na mwendelezo wa maboresho ya taarifa za awali zilizopo kwenye mfumo wa kidigitali wa usajili wa wakulima(FRS).
Vitabu hivi vimetolewa kwa lengo la kupata taarifa za uhakiki wa usajili uliofanyika awali wa  taarifa za wakulima wa korosho kwani taarifa zao ziko kwenye  mfumo wa FRS uliotolewa na Wizara ya Kilimo.

Related posts

BASHE:  BENKI YA USHIRIKA TANZANIA (COOP BANK TANZANIA) KUANZA NA MTAJI WA BILLIONI 55

Amani Ngoleligwe

RAIS DKT. SAMIA KUZINDUA BENKI YA USHIRIKA NCHINI

Amani Ngoleligwe

WAKULIMA WAISHUKURU SERIKALI MFUMO WA TMX

Amani Ngoleligwe