Disemba 31, 2025 04:30
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

LINDI MWAMBAO WAUZA TANI 5,106 KWA BEI YA JUU SH. 2,460 KUPITIA MFUMO WA TMX

Jumla ya tani 5,106 za korosho ghafi zimeuzwa kupitia mfumo wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) katika mnada wa kwanza wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao mkoani Lindi, kwa bei ya juu ya shilingi 2,460 na bei ya chini ya shilingi 2,310 kwa kilo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred amesema mnada huo umefanyika kwa mafanikio makubwa, huku akibainisha kuwa mfumo wa TMX ni mfumo wa uwazi na ushindani katika biashara ya korosho.

Aidha Mkurugenzi ametoa wito kwa wakulima wote kuendelea kuzingatia ubora wa korosho zao kwa kuzikausha vizuri, kwani soko zuri hutegemea ubora wa zao.

Mnada huu umefanyika novemba 9, 2025 ukiwa ni wa pili tangu kuanza kwa minada ya zao la korosho nchini katika msimu wa 2025/2026. Mnada wa kwanza ulifanyika Novemba 8,2025. kupitia Chama Kikuu cha Ushirika Cha Tandahimba na Newala (TANECU).

Related posts

TICC CONFERENCE ANNOUNCEMENT AND CALL FOR PRESENTATIONS

Peter Luambano

ZOEZI LA UHUISHAJI NA USAJILI WA KANZIDATA YA WAKULIMA LAZINDULIWA RASMI

Peter Luambano

MIKOA YA KILIMO CHA KOROSHO KUONGEZEKA KUTOKA 5 HADI 18 NCHINI- Naibu Waziri Silinde

Peter Luambano