Febuari 24, 2026 09:48
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

TIMU YA WAKAGUZI YAKAMILISHA KAZI CBT

Timu ya wakaguzi kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma imekamililisha zoezi la ukaguzi katika taasisi ya Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) kwa jumla ya hoja kumi (10, zoezi ambalo limefanyika kwa muda wa siku nne kuanzia septemba 19 hadi 22, 2025.

Hoja zilizokaguliwa ni pamoja na Ajira mpya, Upandishwaji vyeo, Mafunzo na maendeleo ya watumishi, Nidhamu, Uzingatiaji wa maadili, Anuai za Jamii, Ufuatiliaji wa usalama na afya mahali pa kazi, Usimamizi wa taarifa, utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka, fidia ya magonjwa sugu, na katika hoja hizo, CBT imepongezwa kwa kufanya vema upande wa nidhamu.

Eneo lingine lililofanywa vizuri na CBT ni pamoja na likizo ya mwaka kwa watumishi ambapo watumishi wanaostahili kupata likizo, walipata na walirejea kwa wakati kwenye majumu yao, na taarifa zote kuhusu likizo hufanyiika katika mfumo maalumu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu ndg. Revelian S. Ngaiza, ameshukuru juu ya zoezi hilo na kupokea maoni yaliyotokana na ukaguzi huo pamoja na kuahidi kuyafanyia kazi.

Timu ya wakaguzi hao, imeongozwa na bw. Muhidin A. Muro sambamba na   bi. Hajra H. Mabrouk, bw. Gift S. Lyimo na bw. Florence Mboya.

Related posts

KIAMBATISHO ORODHA YA VIJANA WA KUZIBA NAFASI ZILIZOWAZI.pdf

Amani Ngoleligwe

TAARIFA FUPI YA MINADA YA KOROSHO ILIYOFANYIKA TAREHE 21 OKTOBA, 2023 CHINI YA LINDI MWAMBAO KATIKA KITUMIKI AMCOS-LINDI MC.

Peter Luambano

KIKAO CHA SITA CHA BODI YA WAKURUGENZI WA BODI YA KOROSHO TANZANIA

Peter Luambano