Juni 17, 2025 02:20
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

BODI YA KOROSHO TANZANIA YATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA HUSSEIN BASHE (MB)

Bodi ya Korosho Tanzania yatekeleza agizo la Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe (MB) kwa kutoa vitabu vya kusajili wakulima wa korosho Jimbo la Mtama Mkoa wa Lindi.  Maafisa wa Bodi wametoa mafunzo kwa Maafisa Ugani wa Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Mtama namna ya kujaza taarifa za wakulima ikiwa na lengo na mwendelezo wa maboresho ya taarifa za awali zilizopo kwenye mfumo wa kidigitali wa usajili wa wakulima(FRS).
Vitabu hivi vimetolewa kwa lengo la kupata taarifa za uhakiki wa usajili uliofanyika awali wa  taarifa za wakulima wa korosho kwani taarifa zao ziko kwenye  mfumo wa FRS uliotolewa na Wizara ya Kilimo.

Related posts

UUZAJI KOROSHO KUPITIA TMX WAZIDI KULETA MATOKEO CHANYA

Amani Ngoleligwe

Kikao cha ufunguzi wa zoezi la ukaguzi wa hesabu za taasisi Kwa mwaka 2021/2022

Peter Luambano

SILINDE ASHIRIKI COP29 NCHINI AZERBAIJAN.

Amani Ngoleligwe