Januari 1, 2026 03:58
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

ZIARA YA MASOMO YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAFUNZO YA KILIMO MTWARA-MATI

Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Mtwara wakiwa katika ziara ya masomo ya nadharia Bodi ya Korosho Tanzania,lengo la ziara hiyo ni kujifunza namna Bodi ya Korosho inavyofanya kazi zake hususani upande wa Kilimo.

Katika kufanikisha hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi Ndug. Francis Alfred akiambatana na waataalamu wa Idara mbalimbali kwa pamoja wamewezesha ziara hiyo kwa kutoa ufafanuzi mbalimbali na jinsi Bodi ya Korosho chini ya wizara ya Kilimo inavyotekeleza majukumu yake katika kuboresha na kuendeleza Kilimo cha zao la Korosho Nchini Tanzania ikiwa ni sehemu yaa kukuza uchumi wa Nchi.

Akiongea na wanafunzi hao walioambatana na Wakufunzi wao, Mkurugenzi Mkuu amewaasa kuzingatia masomo yao ili kuleta tija ya elimu waipatayo na kuwa na manufaa kwa jamii watakayo kwenda kuitumikia na kuwa mfano wa kuigwa.

Related posts

TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA

Peter Luambano

ZOEZI LA UHUISHAJI NA USAJILI WA KANZIDATA YA WAKULIMA LAZINDULIWA RASMI

Peter Luambano

BEI YA JUU YA KOROSHO YALETA SHANGWE KWA WAKULIMA KATIKA MNADA WA KWANZA MKOANI MTWARA

Amani Ngoleligwe