Machi 5, 2026 06:15
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

ZIARA YA MASOMO YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAFUNZO YA KILIMO MTWARA-MATI

Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Mtwara wakiwa katika ziara ya masomo ya nadharia Bodi ya Korosho Tanzania,lengo la ziara hiyo ni kujifunza namna Bodi ya Korosho inavyofanya kazi zake hususani upande wa Kilimo.

Katika kufanikisha hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi Ndug. Francis Alfred akiambatana na waataalamu wa Idara mbalimbali kwa pamoja wamewezesha ziara hiyo kwa kutoa ufafanuzi mbalimbali na jinsi Bodi ya Korosho chini ya wizara ya Kilimo inavyotekeleza majukumu yake katika kuboresha na kuendeleza Kilimo cha zao la Korosho Nchini Tanzania ikiwa ni sehemu yaa kukuza uchumi wa Nchi.

Akiongea na wanafunzi hao walioambatana na Wakufunzi wao, Mkurugenzi Mkuu amewaasa kuzingatia masomo yao ili kuleta tija ya elimu waipatayo na kuwa na manufaa kwa jamii watakayo kwenda kuitumikia na kuwa mfano wa kuigwa.

Related posts

TANGAZO KWA WADAU WA TASNIA YA KOROSHO NCHINI

Amani Ngoleligwe

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Francis Alfred, akizungumza na Wakulima wakati wa ufunguzi wa mnada wa kwanza wa ununuzi wa Korosho Msimu 2023/2024 katika Kijiji cha Mburusa Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Octoba 20,2023

Peter Luambano

MADIWANI WA HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA WATEMBELEA MRADI WA KONGANI LA VIWANDA MARANJE

Amani Ngoleligwe