Waziri wa Viwanda na Biashara nchini Mhe. Dkt. Suleiman Jafo amehitimisha rasmi maonesho ya sikukuu ya wakulima (NANENANE) kanda ya kusini – Ngongo mkoani Lindi.
Dkt. Jafo amepongeza mfumo wa stakabadhi ghalani unaotumiwa na wakulima, mfumo ambao ni wenye tija na unalenga kumnufaisha mkulima na jamii kwa ujumla ikiwamo kutoa ajira.
Aidha wizara ya kilimo imeshika nafasi ya kwanza kwenye maonesho haya kanda ya kusini na kwa upande wa mamlaka za udhibiti, Bodi ya Korosho Tanzania imeibuka mshindi wa kwanza kwenye maonesho haya ukanda wa kusini.
Kwa ukanda wa kusini maonesho haya yalifunguliwa rasmi na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala Agosti 1-2025 na yamehitimishwa rasmi na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Jafo Agosti 8-2025.