Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Ndg. Francis Alfred amewataka watumisi wote wa taasisi hiyo kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kukumbuka kujaza majukumu yao kwenye mfumo wa Usimamizi na utendaji kazi katika utumishi wa Umma (PEPMIS) ili waweze kupanda madaraja.
Vilevile, amewataka watumishi hao kuheshimiana na kufuata taratibu za kiutumishi wawapo ndani au nje ya ofisi. Ndg. Alfred Ameyasema hayo wakati wa kikao na wafanyakazi wote wa CBT kilichofanyika tarehe 10 Julai, 2025 katika ukumbi wa mikutano uliopo katika ofisi za CBT makao makuu, Manispaa ya Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara.
Kikao hicho kilichofuatiwa na kikao cha baraza la wafanyakazi kimewakutanisha wafanyakazi wote waliopo Mtwara Makao Makuu na wale waliopo katika matawi yote nchini ambayo ni tawi la Dar es salaam, Mbeya, Katavi, Tunduru, Morogoro, Manyoni, Lindi, Dodoma na Tanga.