Agosti 27, 2025 09:07
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

MAAFISA KILIMO WA BBT KOROSHO WAENDELEA NA MAFUNZO YA VITENDO

Maafisa Ugani Kilimo walioajiriwa na Bodi ya Korosho Tanzania kupitia program ya BBT Korosho waliopo Mtwara – Makao Makuu ikiwa ni moja kati ya vituo tisa vinavyotoa mafunzo, wameendelea na mafunzo ya nadharia na vitendo kama sehemu ya mwendelezo wa mafunzo yao yaliyoanza Januari 13, 2025.

Mafunzo hayo yanahusisha ufahamu wa mbinu bora za kilimo cha korosho ikiwa ni pamoja na udhibiti wa magonjwa na wadudu waharibifu kupitia matumizi sahihi na salama ya viuatilifu ili kuongeza uzalishaji wa korosho nchini. 

Vile vile maafisa hawa wamepata ujuzi kwa vitendo utakaowasaidia kuhamasisha wakulima na kuwasiliana nao kwa ufanisi ili kuboresha zao la korosho.

Mafunzo hayo ni utekelezaji wa programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) iliyopo Wizara ya Kilimo katika zao la Korosho ili kuhakikisha kuwa maafisa hawa wanakuwa na uwezo wa kutoa huduma bora kwa wakulima wa korosho na hivyo kuchangia katika ukuaji wa kipato chao na Taifa kwa ujumla.

Related posts

UHUISHAJI TAARIFA ZA WAKULIMA WA KOROSHO WAENDELEA KWA UFANISI MKUBWA MSIMU WA 2024/2025

Amani Ngoleligwe

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Francis Alfred, akizungumza na Wakulima wakati wa ufunguzi wa mnada wa kwanza wa ununuzi wa Korosho Msimu 2023/2024 katika Kijiji cha Mburusa Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Octoba 20,2023

Peter Luambano

KABRASHA LA MKUTANO MKUU WA WADAU WA TASNIA YA KOROSHO 2025

Amani Ngoleligwe