Januari 27, 2026 11:57
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

SERIKALI YALETA NEEMA KWA WAKULIMA WA KOROSHO


Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) amefanya ziara ya kikazi mkoani Mtwara tarehe 11 Desemba 2025 na kutoa salamu za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa “Serikali itaendelea kuwapunguzia mzigo wakulima wa Korosho kwa kuwa na uhakika wa pembejeo za kilimo.”

Waziri Chongolo ameongeza kuwa Serikali itahakikisha Korosho zote ghafi zinazosafirishwa zitumie Bandari ya Mtwara ili manufaa na maslahi yanayohusisha mchakato wa Korosho yanaacha neema katika mikoa ya kusini.

Akitoa maelekezo kwa Bodi ya Korosho Tanzania, Waziri Chongolo amesisitiza Bodi hiyo kuendelea kulinda soko la awali la Korosho ili kukabiliana na walanguzi holela (maarufu kama kangomba).

Waziri Chongolo ametembelea pia Kongani ya Viwanda iliyopo Maranje ambayo inalenga kuwa na viwanda vya kubangua Korosho ili kuwezesha wakulima kupata tija na thamani zaidi kwenye zao hilo.

Waziri Chongolo pia amesisitiza kuwa kiwanda hicho kiwe na maabara ya kisasa kupima unyevu wa Korosho ili kuhakikisha Korosho zinakuwa bora na shindanishi katika soko la Kimataifa hususan China na Vietnam.

Aidha, Waziri Chongolo amekagua Kituo cha Tafiti za Kilimo cha TARI – Naliendele, na kuwataka watafiti wake kuongeza thamani za ubora wa mbegu na kupunguza visumbufu kwa kuhuisha teknolojia na sayansi katika zao la Korosho, akitolea mfano unyunywizaji wa dawa ya viuwadudu (Sulphur) kwa kutumia teknolojia ya ndege nyuki (drone).

Related posts

UFAFANUZI KUHUSU KIBANDIKO KILICHOWEKWA KWENYE MIFUKO YA SULPHUR YA UNGA CHAPA BENS SULPHUR ILIYOINGIZWA NCHINI MSIMU WA 2023/2024

Amani Ngoleligwe

MWONGOZO NA 1 WA USIMAMIZI WA MASOKO NA MAUZO YA KOROSHO GHAFI KUPITIA STAKABADHI GHALANI MSIMU WA MAUZO 2025/2026

Amani Ngoleligwe

WAKULIMA RUNALI WAUZA KOROSHO KILO 20,630,516 KWA BEI YA JUU TSH 2,610

Amani Ngoleligwe