Juni 22, 2026 03:05
Bodi ya Korosho Tanzania
Habari ZinazojiriKiteleziMatukio

WATUMISHI CBT WAKUMBUSHWA KUJAZA MAJUKUMU YAO KATIKA PEPMIS

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Ndg. Francis Alfred amewataka watumisi wote wa taasisi hiyo kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kukumbuka kujaza majukumu yao kwenye mfumo wa Usimamizi na utendaji kazi katika utumishi wa Umma (PEPMIS) ili waweze kupanda madaraja.

Vilevile, amewataka watumishi hao kuheshimiana na kufuata taratibu za kiutumishi wawapo ndani au nje ya ofisi. Ndg. Alfred Ameyasema hayo wakati wa kikao na wafanyakazi wote wa CBT kilichofanyika tarehe 10 Julai, 2025 katika ukumbi wa mikutano uliopo katika ofisi za CBT makao makuu, Manispaa ya Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara.

Kikao hicho kilichofuatiwa na kikao cha baraza la wafanyakazi kimewakutanisha wafanyakazi wote waliopo Mtwara Makao Makuu na wale waliopo katika matawi yote nchini ambayo ni tawi la Dar es salaam, Mbeya, Katavi, Tunduru, Morogoro, Manyoni, Lindi, Dodoma na Tanga.

Related posts

WAZIRI WA KILIMO MHE.HUSSEIN BASHE (MB) ASISITIZA ZOEZI LA USAJILI WA WAKULIMA WA KOROSHO NCHINI

Peter Luambano

MAPOKEZI YA VIWATILIFU MKOANI MTWARA

Fesam

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Francis Alfred, akizungumza na Wakulima wakati wa ufunguzi wa mnada wa kwanza wa ununuzi wa Korosho Msimu 2023/2024 katika Kijiji cha Mburusa Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Octoba 20,2023

Peter Luambano