KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA, KILIMO NA MIFUGO YATEMBELEA BANDA LA CBT MAONESHO YA NANENANE
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mheshimiwa Deo Mwanyika, agosti 7,2026 imetembelea banda la Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Maonesho vya John Malecela, jijini Dodoma.